ASKOFU MSTAAFU KARDINALI PENGO AFARIKI

 


Kanisa Katoliki Jimbo Kuu Katoliki la Dar es salam limetangaza kifo cha Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, Askofu Mkuu Mstaafu wa jimbo hilo, kilichotokea leo saa 4 usiku wa kuamkia leo Ijumaa, Februari 20, 2026 katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) Jijini Dar es salaam alipokuwa akipatiwa matibabu.

Taarifa iliyotolewa na Askofu Mkuu wa Dar es salaam, Thaddeus S. Ruwa’ichi imeeleza kuwa taarifa za mazishi zitatangazwa baada ya mipango kukamilika.

🕯🪦🕊RAHA YA MILELE UMPE EE BWANA, NA MWANGA WA MILELE UMWANGAZIE, APUMUZIKE KWA AMANI. AMINA

BONYEZA HAPA KUSOMA ZAIDI

#mpembapic📸 

#mpembatv📺 

#newsyoucantrust

Comments